KONA YA UTAMU: Mahusiano
Breaking News
Loading...
Showing posts with label Mahusiano. Show all posts
Showing posts with label Mahusiano. Show all posts

Friday, February 17, 2017

Dalili Muhimu za Mwanamke Aliefika Kileleni Mkiwa Faragha..

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjxE7j-cIycNyO6c_anSbAgugP1lB4vhzXuzbgBIbaRPqguakCaxHzYoFb-uOW2Ps_ITf0GwchqEPG4CMFOF8ZDEjlseyyq0NTR3ECZX6lUySy2bnNmGChB75Xg-vxAKgXEaUpcu8lDg14/s1600/images.jpg
Wanaume wengi sana hua tunadanganywa na wenza wetu kua tumewaridhisha vya kutosha lakini ukweli hua hakuna kitu

Hua wanafanya kwa nia njema tu kwani wanaume hua tunajiskia amani sana kuambiwa umemfikisha mtoto wa kike kwani ni jambo la kishujaa kama trumph uchaguzi us

kwa uzoefu wangu,mwanamke aliefika kileleni hua anakua hivi bila hata kuuliza au kusubili kuambiwa

1.MWILI KUISHIWA NGUVU

mwanamke aliefika orgasm hua anaishiwa nguvu mwili baada ya safari ndefu ya mikito,ukiona baada ya sex msichana anauwezo wa kufanya kazi nzito nzito jua umefanya kazi butu sio mpaka uambiwe

2.KUPITIWA NA USINGIZI BAADA YA MECHI

ukiona ka beby kako kamepitiwa na usingiz gafla baada ya sex jua kaz imeenda sawia,ikumbukwe kufika orgasm ni mechanism inzito,

3.MUSCULAR CONTRACTION

mwanamke anaekalibia/ aliefika kileleni misuli hubana na kuachia ,hii ni kwa mwili mzima hadi kwenye vagina,hilitendo pia hufuatiwa na mwili kutoa jasho.
ukiona ivo ujue kazi zimeenda sawia

Wakuu huu ni uzoefu wangu niliopata nikiwa field,

Ukiona mpenz wako hajaonyesha izo dalili muhimu basi jua hakuna kitu

Kama unajua dalili zingine zile kuu na muhimu tiririka

Wazee Pigeni kazi tutokomeze fake orgasm tunazodanganywa na kupewa kiburi ili tutoe chapaa

Hatua 10 za kumchagua Mchumba

Image result for Hatua 10 za kumchagua Mchumba
Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.
Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi.
Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.
Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli.
Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni vichocheo vinavyowaangusha wengi kwenye mapenzi na wasiowafaa.
Ukweli ni kwamba mtu aliyenaswa kwa ‘ujinga’, huwa hakatwi kiu ya penzi na mwanaume/mwanamke asiye chaguo sahihi la maisha yake. Hivyo hufikia maamuzi ya kujiingiza katika uhusiano mpya mara 2,3,4,5 na kujikuta wakiambulia wanaume/wanawake wale wale wasio sahihi kwake.
Mwanamnke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Suzzy aliwahi kuniomba ushauri, akasema amechoka kuchezewa, maana kila mwanaume anayempata anakuwa si chaguo lake. Lakini kibaya zaidi kuachia ngazi au kutemwa huku akiwa tayari ameshafanya mapenzi na wanaume hao.
Nia ya swali lake ilikuwa ni kuniomba njia za kumtambua mwanaume mkweli bila kufanya naye mapenzi? Aliuliza hivyo huku akiwa na hoja kuwa wanaume wengi hawako tayari kuwa na uhusiano na msichana bila kufanya naye mapenzi na wakati huo huo huficha tabia zao chafu wakilenga kumnasa wamtakaye.
Binafsi nafahamu kuwa kuna wanawake/wanawake wengi ambao hujiingiza katika mapenzi kwa kutekwa na hadaa za mwili na kujikuta wanacheza mchezo wa kitoto wa pata potea.
Ni madhumuni ya somo hili kufundisha vigezo vya kumpata mwanaume/mwanamke halisi wa maisha, bila kufanya naye mapenzi. Njia hii ina faida kwa pande zote mbili yaani kwa mwanamke na mwanaume kwani kuacha au kuachwa bila kufanya mapenzi ni bora kuliko kuwa muonjaji, tabia ambayo huathiri kisaikolojia na ni hatari kwa afya.
Ifuatavyo ni njia ya kisaikolojia ambayo mwanamke anaweza kutumia kumpata mwanaume mwenye kumfaa bila kufanya naye mapenzi tena ni jibu sahihi la kuondokana na mchezo wa kubahatisha kwa wanaume wanaosaka wapenzi wa kweli na si taksi bubu ambazo mchana huweka namba za njano usiku nyeusi.
KWANZA- Ni ya mwanamke/mwanaume mwenyewe kujifahamu na kufahamu vigezo vya mpenzi anayemhitaji katika maisha yake. Ifahamike kuwa kila mwanaume ana wake na kila mwanamke anaye wake wa maisha pia. Hivyo asiyekufaa wewe anawafaa wengine, kinachotakiwa ni wewe kujitambua kwanza ili umtambue umtakaye.
Wanawake/wanaume wengi hawafahamu wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewe na kuumizwa moyo bure.
PILI- Ni kuketi chini na kuorodhesha vigezo stahili vya mwanaume/mwanamke unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.
TATU- Anza kumsaka kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako hutambulika kwa moyo kurithika na mwili kusisimka.
NNE - Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.
Katika uchunguzi huu mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.
TANO - Ajipe muda wa kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha aketi chini na aanze kujumlisha alama za vigezo alivyovijiwekea na jinsi mwanaume huyo alivyopata au kukosa.
Ikibainika mwanaume aliyechaguliwa amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa, basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizikosa anaweza kusaidia kuzikamilisha polepole wakati wa maisha ya ndoa.
Lakini angalizo kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.
SITA - Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka. Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda.
Hata hivyo watalaam wanasema lazima wapenzi wapime umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na mara zote wasaidiane kwa ukaribu.
SABA - Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. Ni ukweli ulio wazi kwamba licha ya wengi kupuuza maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huacha kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana
NANE - Hatua hii ni ya kuweza kuzungumzia ufanyaji mapenzi, hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu hilo na kuamua ufanyaji huo wa mapenzi una lengo gani, kama ni kuburudisha miili basi suala la afya na uzazi salama litazamwe.
TISA - Kutimizwa kwa ahadi ya kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si busara ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.
KUMI - Kuamua kuwa mwili mmoja kwa kuvumilia na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zote za maisha ukiwemo mkwamo na dhiki ambazo huchangia sana ndoa nyingi kuvunjika. Hapa pia ni wajibu wa wanandoa kuchukuliana udhaifu na kusaidia, kuwa tayari kujifunza na kujali zaidi upendo kuliko hisia za mwili ambazo wakati mwingine hudanganya na hivyo kumfanya mwanandoa asivutiwe na mwenzake.
Mwisho ni kwamba kanuni hizi huwafaa watu wazima mapenzi ya kitoto hayawezi kujenga misingi hii imara mara nyingi ni kudanganyana, kuharibiana maisha, kupeana mimba na maradhi

Thursday, February 16, 2017

Michirizi Inayoonekana Kwenye Miili ya Akina Dada Inaashiria Nini?


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiUXm_9b_U2p0JeRuP6hR_gh5lAv01zVQyNh7P5SUTu0jZ_0pxJLZTTnlXCU2yifjML0HMDN4glUdPjOS6y5NRSTgehgZ9jtuIpnGb6lYyqAazUNHDg26yd3DV6BOyac6G6nWtKGyXfinY/s400/Stretch-lines-on-knees-and-behind-knees+%25281%2529.jpg
Hivi Ile michirizi inayoonekana kwa baadhi ya kinadada nyuma ya goti wakiwa wamevaa sketi fupi huwa ni ishara ya utamu wao kama Mwana FA alivyoimba  "Michirizi ya utamu nyuma ya goti mimi hoi na moyo hai sio toi "  au ugonjwa wa ngozi?


Hatua Za Kumgeuza Rafiki Yako Kuwa Mpenzi Wako

Kuna baadhi ya wanaume ambao wanajiskia kuwa na furaha wakiwa na marafiki zao wa kike ambao wanawapenda kisiri, lakini kama umechoshwa na kuboeka kuwa rafiki pekee na mwanamke unayempenda, basi huu ndio wakati mzuri wa kujeuza gemu yako kabisa. Barabara ya kumbadilisha rafiki yako hadi kuwa girlfriend wako inaweza kuwa ndefu, lakini mwishowe huwa na utamu wake. Halafu kama wewe ni mwoga, mpweke, ama bikra ambaye hajui lolote kuhusu jinsi ya kuwatongoza wanawake, basi usitie shaka. Huwa ni rahisi kutimiza hili. Na utaweza kujenga confidence yako na kujeuka mwanaume ambaye anaweza kujumuika na kutangamana na wengine kirahisi. Hii hapa ni njia nzuri zaidi za kukuwezesha kumvutia mwanamke wa ndoto yako na finally ajeuke zaidi ya rafiki yako. Hivi ndivyo unavyopaswa kufanya.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiVJ98lmYmhyphenhyphenS2h_hASqIR16TMr503mBtZGCOrCIvqGPtdERpLivmiAPl3ut22CdV_q0uoWAwlrJNwxLwB_uNgDpEIZygXYLYQVSq0UnYl1JX0_G8YxCc2U0KmpLUUz5g4tWnqsIRrQyoY/s1600/ggggal.jpg

#1 Acha tabia ya kuwa Mr. Mzuri
Ijapokuwa ni vizuri kuwa mwanaume mzuri mara moja au nyingine, kuwa mzuri sana kiasi cha kuwa unaonekana kama unajipendekeza kwa mwanamke hakufai. Mwanzo ukiendelea kumuonyesha uzuri wako kila wakati utabakia kuwa rafiki yake milele. Kama hujawahi kugundua hili, wanawake wengi huwa wanapendezwa zaidi na wanaume ambao ni masharobaro ama ‘bad boys’. Hii ni kwa sababu masharobaro huwa wanaonyesha hulka ya kutojali ama kuwa na hulka ambazo huonyesha ubaya wao mara moja au nyingine – hii huwavutia wanawake sana. Wanawake hupenda wanaume ambao wanaonyesha confidence  – kitu ambacho mwanaume alpha huwa anamiliki. Well, wanaume ambao wanatawala na ambao wanaonyesha kucontrol katika kila hali huwa kikawaida wanakuwa na confidence wakati wote. So, kama utaanza kuiga na kuonekana kama mwanaume sharobaro, unaweza kujeuka na kuonekana na mvuto na nishati zaidi ambayo itakuweka juu katika mashindano kwa muda mfupi sana.

#2 Usimuandame kama kelbu
Kama unapenda kumfuata fuata mwanamke kama kelbu, basi ataudhika na wewe na mwishowe atakuacha katikati. Mbaya zaidi anaweza kuambia marafiki zake kuwa wewe ni fala usiyekuwa na kazi ya kufanya. Ama anaweza kukatiza urafiki wenu. So, njia nzuri ya kufanya kwa sasa ni kurelax na utulize gemu. Kwa njia nyingine ni kuwa, usimkimbize kufanya jambo lolote. Ukitaka kumfanya mwanamke awe interested na wewe  kiharaka ni kwa kuhakikisha ya kuwa unakuwa mtu asiyeeleweka, yaani leo uko na yeye, kesho uko busy hupatikani. Huku kutamfanya akumisi na kutaka kuspend muda wake mwingi na wewe.

#3 Usikubaliane na kila kitu
Kama utaendelea kufanya kila kitu ambacho mwanamke anakuambia ama kukubaliana na kila kitu anachotaka, basi ataanza kukuchukulia advantage kwa sababu atagundua kuwa amekuweka katika viganja vyake. Jithamini wewe mwenyewe zaidi kuanzia sasa na umuonyeshe kuwa haubabaikii ama kuomba atenshen kutoka kwake. Hii itamfanya kuanza kujishuku na itamfanya kutaka kujua kwa nini umekuwa tofauti. Baadaye, ataanza kukukimbilia ili abadilike.

#4 Isome na uielewe sanaa ya kutongoza
Katika dunia ya kudeti na kutongoza, hakuna kitu kinachofanya kazi vizuri zaidi kama kushawishi. Mwanzo, hakuna kitu ambacho kitatokea kati yako na rafiki yako kama hujui kushawishi. So, nenda ujifunze jinsi ya kutumia macho yako kumtongoza rafiki yako, mpe tabasamu, mfinyie jicho, na mhusishe katika gumzo ambalo litampa hamu ya kukukaribia. Fanya haya yote na utaona utofauti wa rafiki yako akianza kufall na wewe pole pole. Utajipata rafiki yako amejeuka kuwa mpenzi wako.

Maswali 40 Ya Kumuuliza Mwanamke Katika 'Date'


Ushawahi kutoka deti na mwanamke halafu ukafikia mahali katika chat yenu unaishiwa na maneno ya kuongea?

Ama umeagana na mwanamke mtoke deti siku ya pili halafu umekuwa ukikesha siku nzima ukiwaza ni maneno ama ni usemi gani utakaoongea siku ya pili wakati ambapo mtakutana?
Image result for date outings
Well, usiogope. Hapa umefika kwa zahanati ambayo itakutibu matatizo yako.

Hapa tumekuandalia maswali 40 ambayo utayatumia kumuuliza mwanamke na kuyafanya maongezi yenu yavutie na kumfanya mwanamke apendezeke na wewe hadi mwisho.

Well. Kabla ya kuorodhesha maswali haya kuna mambo ambayo unapaswa kufahamu:

  • Anza kwa kumsifia ama kumpendezea kwa mambo anayofanya mfano unaweza kumsifia vile alivyovalia, kazi yake, umbo lake nk.
  • Wakati utakapokuwa unamuuliza mwanamke haya maswali, hakikisha ya kuwa unatoa nafasi ya angalau sekunde 30 kabla ya kumuuliza swali la pili, yaani usimmiminie maswali yote wakati mmoja.
  • Hakikisha kuwa haulazimishi maswali yako, mwanamke akikataa kujibu swali lako jipe shughli kiasi kv unaweza kucheza na vidole vyako ama jambo jingine kabla kumuuliza swali lingine.
Baadhi ya mambo ambayo pia unapaswa kuzingatia katika rodha ya maswali haya ni kuwa:

Unapaswa kuyachanganya maswali yako. Maswali tuliyoyaorodesha hapa ni maswali yaliyowazi, yaani yanaweza kupanuliwa yakazua mada nyingine. Anza na maswali sahili kuangalia iwapo mwanamke unayezungumza naye anapenda kuongea au la. Pia muulize maswali yaliyo wazi ili kuongeza hoja yako.

Usimakinike na orodha ya haya maswali. Tumia maswali machache ambayo unayaona unaweza kuyatumia halafu ujeuza mada yako uanze kuongea maswala yako. Ukimakinika kutaka kutumia maswali haya yote basi unaweza kumfanya akuone hauvutii na anaweza kuboeka na wewe haraka sana.

Usihifadhi maswali haya. Hili ndilo jambo baya zaidi la kufanya. Ukikaa na deti wako huku ukirudia swali la kwanza hadi jingine unaweza kumfanya mwanamke aone kwamba unamfanyia mahojiano ya kazi. Unachohitajika ni kusoma baadhi ya maswali haya, yahifadhi kwa simu yako halafu yatumie wakati ambapo maongezi yako yanafifia.


Maswali yenyewe ni kama ya fuatayo...

1. Unaipenda hii sehemu?

2. Huwa unapenda kunywa kinywaji gani?

3. Mapochopocho unayoyapenda ni yapi?

4. Ushawahi kuja hii sehemu awali?

5. Siku yako ilikuwaje?

6. Unafanya kazi wapi?

7. Huwa unapenda nyimbo aina gani?

8. Unapenda salad aina gani?

9. Ni mkahawa gani unaoupenda zaidi?

10. Ni movie aina gani unapenda kuangalia zaidi?

11. Ni mambo gani unapenda kufanya baada ya kutoka kazini?

12. Unafanya mambo gani ili kujifurahisha?

13. Ulisomea wapi?

14. Sehemu gani unaipenda sana zaidi kwa likizo zako?

15. Ni kitu gani unapendekezea ili kuinjoy siku yako?

16. Je wewe ni mtu wa kufuga mnyama gani? Paka ama mbwa?

17. Kama ungetawala dunia, ungetaka kubadilisha kitu gani?

18. Mapenzi mazuri ni yapi kulingana na mtizamo wako?

19. Mzazi gani yuko karibu na wewe?

20. Ni kitu gani kinachokuboa kwa mwanaume?

21. Unapenda kuvalia kikazi ama kimtaa?

22. Unawachukuliaje wanawake ambao wanapenda maringo?

23. Hivi ni kweli kuwa wewe unakuwa mrembo hivi?

24. Je wewe ni mtu wa kusoma ama wapenda kucheza games?

25. Ni mtu gani katika maisha yako ambaye unampenda zaidi?

26. Unapenda mambo ya ghafla ghalfa ama mpangilio?

27. Ni nani huwa unaongea naye kama unapata changamoto katika mapenzi?

28. Je una kumbukumbu yeyote ya utotoni mwako ambayo inakufanya utabasamu unapoifikiria?

29. Ukisafiri katika hii dunia, ungetamani usikose nchi ngapi tano?

30. Ni kitu gani kinakufurahisha maishani mwako?

31. Je, wewe uko karibu na familia yako?

32. Ni kitu gani unachochukia zaidi kuona wakati unapokutana na deti wako mara ya kwanza?

33. Je wewe ni mtu wa kurauka mapema ama kuchelewa usiku zaidi?

Haya yafuatayo ni baadhi ya maswali ambayo unaweza kumuuliza deti wako iwapo ameingiliana na mazungumzo yako. Maswali haya yanaweza kuwa ya ucheshi, mengine yanaweza kuchangia kuongeza mazungumzo na baadhi yanaweza kubashiri vile ambavyo deti yako itakuwa mbeleni na huyu mwanamke.

34. Ni sehemu gani ya mwili wako huwa inatekerenyeka zaidi ikiguswa?

35. Ulikuwa miaka mingapi mara ya kwanza ulipohisi kupenda mtu flani?

36. Ni kitu gani kinachofanyika kawaida unapokuwa na marafiki zako wa kike mkiwa mnapokula bata?

 37. Kimtizamo wako, maana ya mahusiano ni nini?

38. Hivi, mahusiano yako ya awali yalichukua muda gani?

39. Deti yetu ya leo umeiona vipi kabla tumeet tena wakati mwingine?

40. Sahizi unafikiria nini?

SOMA: FAIDA YA KUNYONYWA UUME WAKATI WA TENDO LA NDOA

Pata mchumba, mpenzi! Click Hapa

Karibu sana msomaji wangu kila siku upate mbinu mbali mbali za kukuondolea aibu katika mahusiano yako. Ukijenga utamaduni wa kutembelea mtandao huu kila siku muda si mrefu unakuwa tajiri wa mahaba pamoja na kuwa na mahusiano thabiti sana. Kazi kwako!

Tuesday, February 14, 2017

JE,UKE WAKO UNATOA HARUFU MBAYA..? JINSI YA KUMALIZA TATIZO LAKO

Image result for harufu mbaya ukeni
Tatizo la uke kutoa harufu mbaya ni tatizo linalowasumbua wanawake wengi.


Wanaume wengi kila kukicha huwa wanalalamika kuwa inaboa na inakera kupeana Raha na Utamu na Mwanamke ambae sehemu zake za siri zinanuka. Inawatoa out of the mood, mwisho wake wanaconcetrate kudo fasta, wamalize hamu zao kila mtu aondoke.

Wapo baadhi ya wanawake wanajijua wanasumbuliwa na hili tatizo lakini cha kushangaza hawana muda wa kutafuta solutions za kumaliza tatizo lao (wanaishia kuchekwa kuwa vituko vya mtaa bila kujijua bcoz hawajui kuwa matatizo yao ya uke kutoa harufu mbaya,yanasimuliwa na wale wanaume ambao washawahi kulala nao wakiwa wanapiga story na marafiki zao maskani mtaani).

lakini wapo wanawake wachache wenye busara,ambao wanajijua wanasumbuliwa na hili tatizo na wangependa kujua sababu na jinsi ya kulimaliza,na hao ndio wamenifanya mie niandike hii post
Nitaanza kuelezea sababu kisha nitaelezea ni jinsi gani unaweza kumaliza tatizo lako.

Sababu zinazosababisha uke kutoa harufu mbaya ni kama zifuatazo,

1.BACTERIAL VAGINOSIS
Kwa mujibu wa madaktari bingwa,inasemekana kuwa hili ndio tatizo namba moja linalosababisha uke kutoa harufu mbaya.Inawezekana ukawa msafi mpaka mwisho lakini ukisumbuliwa na hili tatizo basi lazima uke wako utatoa harufu mbaya.

Kila uke una bacteria ambao wapo naturally kwa ajili ya afya njema ya uke wako,Lakini kama ikitokea hawa Bacteria wakazidi na kuwa wengi kupita kiasi ambacho uke wako unaweza kuhimili ndio hapo hiki kitendo kinaitwa Bacterial Vaginosis.

Sababu zinazosababisha Bacterial Vaginosis hazijulikani kwa usahihi lakini madaktari wanasema inaweza ikasababishwa na kitendo cha kupeana Raha na Utamu bila condom especially kama vitu vilivyoingia kwenye uke wako wakati wa kupeana Raha na Utamu vilikuwa vichafu(vitu kama vidole au mashine ya mwanaume,or may b dildo etc) au mara nyingine inatokea naturally bila sababu.

Ukitaka Kujua kuwa unasumbuliwa na Bacterial Vaginosis,utajikuta unapata Dalili zifuatazo;

  • Uke kutoa maji maji mazito au mepesi yenye rangi ya njano(yellow) au Brown yenye harufu mbaya
  • Maumivu kwenye maeneo ya kiuno au nyonga
  • Unaweza usipate au ukapata maumivu ya kichwa.
  • Uke wako unaweza ukawa unawashwa au usiwashwe (ur vagina might itch or not)


2. YEAST INFECTION
Hili Pia ni Tatizo,lipo kama la Bacterial Vaginosis.tofauti yake ni kuwa kwenye Bacterial Vaginosis waliokuwa wamezidi ni bacteria lakini huku wanaozidi ni fungus candida albicans. Ni wanawake wachache huwa wanapata Bacterial Vaginosis lakini wanawake wengi lazima wapate Yeast Infection japo mara moja katika maisha yao.

Mara nyingi Yeast Infection hutokea Naturally au inaweza kusababishwa na aina ya vyakula au vinywaji unavyokula au kunywa especially kama vimejaa yeast(vyakula vyote vinavyotengenezwa na hamira,pombe etc) Ukitaka kujua kama unasumbuliwa na Yeast Infection,utajikuta unapata Dalili zifuatazo;

Uke wako ukawa unawashwa au usiwashwe (ur vagina might itch or not) Maumivu kama uke unaungua pale unapokuwa unajisaidia haja ndogo (when u pee) Uke kutoa maji maji mazito yenye rangi nyeupe kama jibini(cottage cheese)


3. SEXUALLY TRANSMITTED DISEASES (STDs)
Kuna baadhi ya magonjwa yanayosababishwa na kupeana Raha na Utamu bila Condom,kama vile Chlamydia na Gonorrhea(kaswende na kisonono),kama ukiyapata huwa yanasababisha Uke kutoa Harufu mbaya kwa sababu dalili zake zinahusiana na kutokwa na maji maji yenye harufu mbaya.

4. VAGINAL OR CERVICAL CANCER
Unapokuwa una kansa ya uke au kansa ya mlango wa kizazi(cervical cancer),kutokwa na maji maji yenye harufu mbaya ni sehemu ya dalili zake.Unapojiona kuwa una tatizo la uke kutoa harufu mbaya,ni heri na itakuwa busara ukienda hospitali,kama ni kansa ya mlango wa kizazi itakuwa sio ngumu kuitibu kama ukiwahi mapema.

5. POOR HYGIENE
Inawezekana pia tatizo la uke wako kunuka linasababishwa na uchafu. May b unaoga mara moja tu kwa siku au siku nyingine hata hauogi. Hauna mazoea ya kufua nguo zako za ndani(underpants),na ikitokea siku umezifua basi hata hauzisugui zikawa safi.n.k

MAMBO UNAYOTAKIWA KUFANYA UKITAKA UKE WAKO USITOE HARUFU MBAYA

1. OSHA UKE WAKO KWA MAJI SAFI KILA UNAPOMALIZA KUJISAIDIA HAJA NDOGO(PEE)
Asilimia kubwa ya wanawake hawana mazoea na utaratibu huu.Ni utaratibu muhimu katika maisha ya kila siku ya mwanamke. Unapokuwa unajisaidia haja ndogo,most of the tym lazima utakuwa umechuchumaa/umechutama(umesquat),haja ndogo yako inapokuwa inatoka,lazima kutakuwa na mabaki kidogo kidogo yatakurukia na kubakia kwenye lips za nje au za ndani za uke wako(labia majora or minora).

Hayo mabaki baada ya muda yatachanganyika na jasho(sweat) na kutengeneza harufu mbaya,kwa hiyo ili kujiepusha na yote haya,ni heri ukaosha uke wako kwa maji safi kila ukimaliza kujisaidia haja ndogo.

2. UKIWA UNAOSHA SEHEMU ZAKO ZA SIRI,TUMIA MTINDO(STYLE) WA KUPELEKA MKONO KUTOKA MBELE KURUDI NYUMA
Kuna baadhi ya wanawake teyari wameshazoea kusafisha sehemu zao za siri kwa kupeleka mkono kutoka nyuma kuja mbele.Huu mtindo sio mzuri kiafya kwa kuwa huko nyuma kuna Tigo (anus), na kwenye Tigo kumejaa uchafu na bacteria wengi tu.Sasa wakati unajisafisha,unapopeleka mkono nyuma unakuwa kama unazoa bacteria na uchafu kutoka kwenye Tigo,halafu ukauleta mkono mbele unakuwa unawaacha hao bacteria na uchafu kwenye uke wako. Na huo ndio mwanzo wa uke wako kutoa harufu mbaya na kupata infections za ajabu ajabu.

Ukitaka kuwa salama,haijalishi kuwa umemaliza kujisaidia haja kubwa au ndogo,au wakati unaoga,ukitaka kusafisha sehemu zako za siri,tumia mtindo wa kupeleka mkono mbele kurudi nyuma ili usije kuwaleta bacteria na uchafu wa Tigo mbele.

3. VAA NGUO ZA NDANI ZENYE ASILI YA PAMBA(COTTON)
Pamba(cotton) ina uwezo wa kupitisha hewa hata kama ni kidogo sana. Na sehemu za siri za Mwanamke zinahitaji flow ya hewa inayopita,nyingine iwe inaingia na nyingine iwe inatoka.Hii flow ya hewa hata kama ni ndogo itasaidia kufanya sehemu zako za siri kuwa fresh muda wote na utapunguza uwezekano wa uke wako kutoa harufu mbaya.

Na pia punguza kuvaa nguo za kubana sana muda wote,nguo za kubana zinasababisha majasho sehemu za siri na ukizingatia hamna flow ya hewa kwenye sehemu zako za siri basi lazima hayo majasho yataanza kutoa harufu mbaya.

4. USIVAE NGUO YA NDANI MOJA SIKU NZIMA
Kwa jinsi maumbile ya Mwanamke yalivyo,unatakiwa kubadili nguo ya ndani mara mbili au tatu kwa siku.

May b ulivaa nguo ya ndani asubuhi,ikifika mchana,ingia ladies room(bafuni/chooni),Vua Nguo yako ya Ndani,kisha unaweza ukaoga mwili mzima(which is better) au ukasafisha sehemu zako za siri.Nguo ya ndani uliyovua unaweza ukaifua(which is better) au ukaikunjakunja na kuiweka ndani ya kipande cha khanga au kitenge ndio uweke kwenye handbag yako ili kama ikitokea ukaopen handbag yako in public,watu wataona khanga au kitenge,hawatojua ndani umeweka nini.

5. PUNGUZA KULA VYAKULA VYENYE SUKARI AU YEAST KWA WINGI
Unaweza ukapunguza uwezekano wa kupata Yeast Infection au Bacteral Vaginosis kwa kuacha au kupunguza kula vyakula vyote vyenye sukari au yeast kwa wingi.

Vyakula hivyo ni kama vile vyakula vyote vinavyotengenezwa na hamira,pombe/bia n.k
Ukizidisha Vyakula au vinywaji hivi,ina maana utakuwa unazidisha yeast mwilini,na wakizidi kwenye uke utapata yeast Infection,mwisho wake uke wako utaanza kutoa harufu mbaya.

6. BADILI PADS ZAKO MARA KWA MARA UNAPOKUWA KWENYE SIKU ZAKO
Ili kuzuia uke wako usitoe harufu mbaya kipindi ambacho upo kwenye siku zako,inashauriwa kubadili ur pad mara kwa mara(may b after each 4 or 6 or 8 hours,it will depend how many pads can u afford per day) Kubadili pads mara kwa mara kunasaidia ujisikie upo comfortable,inazuia bacteria kujikusanya,inasaidia kupunguza uwezekano wa kupata infection na mwisho inaondoa uwezekano wa uke wako kutoa harufu mbaya.

7. NYOA (SHAVE) NYWELE ZAKO ZA SEHEMU ZA SIRI MARA KWA MARA
Nywele zako za sehemu za siri zinapokuwa ndefu,unakuwa umetengeneza maficho(hiding place) ya kila aina ya uchafu kuanzia jasho,majimaji yatakayokuwa yanakutoka ukeni ukiget aroused,mabaki ya haja ndogo n.k Ili kuepusha yote haya ni heri ukawa unazikata nywele zako za sehemu za siri mara kwa mara.

8. NENDA HOSPITALI MAPEMA NA HARAKA TENA SANA
Yaani hata usichelewe,kwani haya matatizo especially Bacteral Vaginosis na Yeast Infection ni matatizo ambayo yanaweza kutibika kwa dawa.Ni heri uwahi mapema ili uongeze uwezekano wa kupona haraka bila matatizo.

Saturday, December 10, 2016

Sifa 10 za Mtu Mwenye Penzi la Kweli Kwako....

Vijana wengi ambao wanapendana leo mapenzi yao hayadumu kiasi cha kubatizwa jina la utamu wa bazoka. Lakini yote hii inatokana na ukweli kwamba elimu ya mapenzi ambayo ni muhimu kwa binadamu haitolewi ipasavyo.

Ipo zana potofu kwamba kumfundisha mtoto mapenzi ni kumharibu, jambo ambalo si kweli bali inategemea mtoto huyo anafundishwa nini na kwa wakati gani. Lakini cha kushangaza zaidi hata watu wazima ambao ni wadau wa mapenzi hawayajui, matokeo yake wanajiingiza kwenye uhusiano wakiwa bumbumbu na hivyo kuteshwa na changamoto zinazowakabili.
Leo tutajifunza kwa undani sifa kumi za mpenzi bora ili tuweze kuwatambua wapenzi wetu kabla ya kuwapa mioyo na utu wetu. Sifa hizo ni hizi zifuatazo.

1.Mpenzi wa kweli ni yule ambaye hatangoja kujua nini unahitaji yaani hana sababu ya kusubiri kuombwa ndiyo atoe msaada.

2. Ni yule atakayejua wakati gani huna furaha au una furaha na atakuwa na wewe kwa hali zote mbili .

3. Ni yule atayekuwa tayari kukusikiliza kwa kile utakachosema, hatojali umeongea baya au zuri

4.Atakuwa na wewe wakati wa shida na raha. Hatakuwa mtu wa kuvizia vizia na kujisogeza wakati ukiwa na raha.

5. Mpenzi wa kweli atakuheshimu na hatopenda kuwa kikwazo cha maisha yako, atakulinda daima.

6. Atakupenda kwa moyo wake wote na wala si kwa ajili ya shinikizo fulani (pesa au mali)

7. Mpenzi wa kweli ni yule atakayeonyesha kuthamini nafasi yako kama rafiki au mpenzi mbele ya wengine, hafichi hisia zake mbele za watu, atakutetea na kukufanya wa kwanza.

8. Kwenye ukweli mpenzi mzuri atasema bila kukuficha na atapenda kukuonyesha mifano ya namna ya kuwa mkweli na mwaminifu.

9.Mpenzi wa kweli ni yule anayejiamini, asiyeyumba katika maamuzi hata kama atalazimika kufanya maamuzi magumu .

10.Atakuwa tayari kuvumilia, hatakuwa mwepesi wa hasira wala kutumia lugha chafu na ubabe.

Sunday, December 4, 2016

Jinsi Ya Kuzungumza Na Mwanamke Ili Umvutie

https://encrypted-tbn2.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcThNM32QiyhJalDZgcfaurxKCCM0ZVsjlXH0sBCnGxsf2kKkLWC
Kama unatabia ya kushindwa ama kupata tatizo la kuongea na wanawake ambao wanakuvutia, basi ni wakati murua wa kwako kutafuta mbinu ambayo itakufanya wewe kuwa na ari na kutokuwa na wasiwasi wowote wakati ambapo unaongea nao.
Wakati mwingine, wanaume hujiskia ndivyo sivyo wakati wanapoongea na wanawake na mara nyingi wanapalia kutoongea na wao kabisa kwa sababu ya kujiskia ndivyo sivyo. Hii mwishowe inachangia kwa wao kutoweza kuwafahamu wanawake vizuri ama kushindwa kuwatoa date. Kama umechoshwa na jambo hili ambalo linakuandama siku nenda siku rudi, basi unahitaji njia rahisi ya kukuwezesha wewe kuzungumza na wanawake na kuyafanya maisha yako rahisi. Kama kumtoa mwanamke date sahizi ni jambo gumu kwako, basi unafaa kujua kuwa hilo halifai kuwa tatizo lako kamwe tena.

Hii hapa ndio njia rahisi ya kuongea na mwanamke ambayo itakusaidia kupata ujuzi kadri muda unaposongea.

1. Usijaze mazungumzo yenu na kwa kumsifu saana.
Kuna makumi ya wanaume katika nyanja hii ambao wanapenda sana kutumia maneno ya kumsifu mwanamke kama wameishiwa na maneno wakati wanapoongea na mwanamke. Wanaume wengine hufanya hivyo ili kudhihirisha kwa mwanamke kuwa wamevutiwa nao. Lakini makosa ni kuwa, kutumia maneno ya kumsifu mwanamke hayaongezi sana wala hayafanyi mengi kumsaidia mwanamke. Kwa hivyo, weka maneno ya kusifu kando, na uanze kuongea mambo mengine ambayo yatamvutia pia. Kama hutafanya lolote kando na kumwambia kuwa umemzimia kwa urembo wake au macho yake, utakuwa umejiweka level moja na wanaume wengine ambao wanatumia mitindo io kwa hio.
Kumbuka: wewe unawezekana kuwa si mwanaume wa kwanza ambaye umevutiwa naye. Mwanzo, kuna uwezekano mkubwa kuwa wanaume wote wanamuona yeye anavutia. Hii inamaanisha kuwa kumsifu wewe kwake haitakuwa jambo geni kwake.

2. Usijikite sana kuonyesha ya kuwa unamwona yeye anavutia
Kusistiza, ni kuwa haufai kuweka akili yako ijikite kuwa unamwona mwanamke unayeongea naye anavutia kupindukia. Ukijisahau tu ukianza kumfikiria vile ana urembo na kuvutia, utakuwa unajipa presha ambayo haitakuwa na manufaa yeyote kwa mazungumzo yenu. Kuna njia rahisi ya kuepuka jambo hili, ni kuwa unafaa kuidanganya akili yako kuwa huyo mwanamke unayeongea naye hana urembo wowote ule. Presha ikishuka katika mwili wako, utajiona umepata fursa rahisi ya kuweza kujieleza ukiwa pamoja na mwanamke yeyote yule.

3. Tafuta mambo ambayo munagawa kimaisha
Ok, haitakuwa jambo gumu vile mkianza kuongea mambo ambayo mnagawa ama intrest ambazo mnashare. Mwanzo kama mtaanza kuongea mambo ambayo mnagawa katika maisha, itakuwa ni njia rahisi ya wewe kuweza kupata namba yake ya simu ili kuweza kumshawishi kumtoa date.
Kumbuka: mwanamke akigundua kuwa mnashare intrest pamoja, hapo hapo atataka kuutumia muda wake zaidi mkiwa pamoja ili mpate kuzungumza intrest mnazoshare. Hivyo basi, fanya utafiti wa kina na ujaribu kuvumbua jinsi na njia utakayoitumia ili muweze kujumuika pamoja.

SOMA: Utamgunduaje mwanamke aliekwisha zaa mtoto wakati wa mechi??

Pata mchumba, mpenzi! Click Hapa

Karibu sana msomaji wangu kila siku upate mbinu mbali mbali za kukuondolea aibu katika mahusiano yako. Ukijenga utamaduni wa kutembelea mtandao huu kila siku muda si mrefu unakuwa tajiri wa mahaba pamoja na kuwa na mahusiano thabiti sana. Kazi kwako!
 
 

Saturday, December 3, 2016

Kwa Nini Wanawake Wanapenda Wanaume Masharobaro aka Bad Boys


http://scontent.cdninstagram.com/t51.2885-15/s480x480/e35/13269538_108792916207153_1590634045_n.jpg?ig_cache_key=MTI1NjQzNzIyNzQ3NTA2NDczNA%3D%3D.2Wanawake kuchagua wanaume masharobaro aka badboys kuwaliko wanaume wa kawaida si jambo geni na hutokea mara kwa mara. -aidha katika vyuo, vilabuni, sinema, maktabani ama sehemu yeyote ile. Wanaume masharobaro, kama wanaume wengine, wao pia wanamaumbo ya kila aina, shepu na mvutio wa kijinsia. Kama wewe ni mwanamume wa kawaida ambaye humaliza wa mwisho ama ushawahi kupoteza mpenzi wako kwa sharobaro fulani, hapo chini kuna nadharia ambazo zitasaidia kueleza kwa nini  wanawake wanapenda sana kuvutiwa na wanaume masharobaro.

1. Hamu ya kufuata
Kufuata kitu ambacho unakipenda huwa kuna msisimko fulani mtu hupata. Lakini msisimko zaidi hutokea wakati ambapo mtu anajaribu kufuata mtu ambaye hataki kujulikana mienendo yake ya kimaisha, kufuatwa ama kueleweka kimaisha. Haya ndio maisha anayoishi mwanamume sharobaro. Wanawake wanapenda sana wanaume ambao hawaeleweki kimaisha (yaani hawatambuliki) ama kutaka kujua maisha yao. Na wewe kama mwanamume unataka kutumia huu udhaifu kwa manufaa yako, wakati mwingine unafaa kumfanya mwanamke abaki na maswali chungu nzima kutaka kukujua zaidi. Kama unampenda, jaribu kadri iwezavyo kutojaribu kumuonyesha.  Badala yake mpe pia yeye changa moto kwa kuweka ujanja wa kutoeleweka mara kwa mara. Hii ni njia moja murua ya kuhakikisha utaingia katika akili yake.

2. Kutaka kuwafunga fundo
Kitu kingine ambacho wanawake huvutiwa kwa sharobaro ni kutaka nafasi ya kuwafunga fundo ama kuwajeuza tabia zao. Mwanamke, amezaliwa naturally na hisia za uzazi, yaani kutaka kujeuza mtu mwenye tabia ovyo kuwa na tabia nzuri. Hii huibua hisia halizi za uzazi ndio maana kama mwanamume unapaswa wakati mwingine kumsumbua mwanamke hikisia, kimawazo na kadhalika. Unafaa kuwa mpinzani lakini usiwe mhalifu. Unafaa kuwa hatari lakini usipitishe kiwango ambacho kitamwogopesha. Kimtazamo, unafaa kumfanya mwanamke auonyeshe uke wake wote ili kujaribu kukubadilisha, mpe nafasi ajaribu kuubadilisha upande wako wa kiza na mwishowe kukufanya uwe mwanamume thabiti katika mchakato mzima.

3.Uanaume uliothabiti
Wanaume masharobaro (na si wale feki) karibu nyakati zote huwashinda wanaume wa kawaida kwa sababu ya mambo mawili makuu. Kwanza ni kuwa ni wanaume majasiri na pili wanaudhibiti uanaume wao kwa kuwa ngangari kimaisha. Kutoogopa kwao kwa jambo lolote ndiko kunawafanya wanawake kuvutiwa nao. Wanawake wengi wanavutiwa na wanaume ambao ni hatari, ngangari na wenye nguvu kwa sababu si rahisi kuchezewa au kufanyiwa masihara. Ukismama  kumtetea mwanamke kuhusu mahitaji yake na uovu, hii inamaana ya kuwa una uwezo wa kusimama kando yake na jambo lolote lile.  Kuweza kuonyesha level ya kuwa wewe ni mtu usiekuwa na woga wowote, unafaa kumwonyesha mwanamke wako kuwa una uwezo wa kuwa ngangari mahali popote pale ili mradi kumlinda yeye tu.

4. Uoga wa kujitwika majukumu
Wanaume masharobaro hupenda kuhepa majukumu yanayohusiana na mahusiano. Kwa wanawake ambao wana uoga huo huo wa kuwa na majukumu, masharobaro huwavutia sana na kuwaona kama hakuna wanaume wazuri kama hao. Kwa kuwa wanawake hawatajitweka majukumu, huwa hawana haja ya kujishughulisha na hisia za kipenzi ambazo ni stress. Pia ni habari njema kwa wanawake ambao wako tayari kwa uhusiano wa kimapenzi wa muda mfupi pekee. Lakini kama kawaida, mwisho wa siku lazima mwanamume sharobaro au mwanamke mtundu lazima kuna sehemu fulani ndani ya mawazo yake anatamani kuwa na mahusiano ya kudumu na pia kupendwa. Hivyo siri hapa ni kuipima miondoko yake na uangalie level yake ya kujitwika majukumu katika mapenzi halafu sasa uanze na hapo.


Upende usipende, wanaume masharobaro watakuwa na nafasi kubwa katika moyo wa mwanamke. Kuna kitu ndani yao ambacho kinawasababisha wanawake kuangua mwili mzima kihisia na kimapenzi kwao. Lakini hii haimaanishi kuwa lazima kila mwanamume ajeuke na kuwa sharobaro ili aweze kuwa na nafasi rahisi ya kutongoza mwanamke aliye kwa ndoto zako. Kile unachotakiwa kufanya ni kucheza mchezo mzima kiwastani. Daima unafaa kuwa vile ulivyo huku ukiingiza tabia flani za usharobaro hivi katika miondoko yako. Kama kuna kitu nzuri kati yenu wawili, basi pia kuna sehemu mbaya ambayo unaweza kuitumia ili ukajinufaisha nayo


SOMA: FAIDA YA KUNYONYWA UUME WAKATI WA TENDO LA NDOA

Pata mchumba, mpenzi! Click Hapa

Karibu sana msomaji wangu kila siku upate mbinu mbali mbali za kukuondolea aibu katika mahusiano yako. Ukijenga utamaduni wa kutembelea mtandao huu kila siku muda si mrefu unakuwa tajiri wa mahaba pamoja na kuwa na mahusiano thabiti sana. Kazi kwako!